Tuesday, December 25, 2012

Marry Christimas

Ndugu zangu wapendwa  karibuni katika maadhimisho ya Sikuku ya Christmas na tujumuike na tuweze kuitumia siku hii ya leo vizuri

Friday, December 21, 2012

RUHUSU MAPENZI YA MUNGU YATIMIE KUHUSU MWENZI WA MAISHA YAKO.



Najua yumkini upo njia panda kwa habari ya kuoa au kuolewa. Si kwa sababu hakuna mtu wa kuoa au kukuoa, bali ni kwa sababu kila anayekuja ni tofauti kabisa na kile ambacho wewe unapenda na unafikiri pia ni mapenzi ya Mungu iwe utakavyo. Huenda kibinadamu kuna sifa/vigezo ambavyo ulijiwekea vya mtu ambaye ungependa kumuoa au kuolewa naye, lakini kila unapoomba unaona mtu anayekuja ni tofauti kabisa na vile ulivyotaka wewe. Na unapoomba zaidi kumhoji Mungu anakuhakikishia kwamba huyohuyo ndiye mtu wa mapenzi yake.
Hukuishia hapo umeshirikisha na wapendwa wenzako au hata watumishi wengine wameomba nao wamethibitisha huyo ndiye mtu wa mapenzi ya Mungu kwako. Kila unapojitahidi kufikiri kumwacha unakosa amani. Mimi ninakushauri inapofika mahali kama hapo we ruhusu tu mapenzi ya Mungu yatimie kwako. Zipo sababu nne za msingi  zinazonifanya nikushauri hivyo;
  • Mapenzi ya Mungu ndio utimilifu wa kusudi lake kukuleta wewe duniani.
Haukuja duniani kwa sababu ni kawaida ya wanadamu kuzaa, bali ni kwa sababu ni Mungu alikusudia wewe uzaliwe.Hii ina maana lipo kusudi la Mungu kukuleta duniani. Na ili kusudi lake liweze kufikiwa ni lazima ujifunze kuishi maisha ya mapenzi yake. Uishi ili kutimiza mapenzi yake hapa duniani.
Ni mapenzi ya Mungu pia kuhakikisha unaoa/kuolewa na mtu ambaye anajua mtasaidiana katika kutekeleza makusudi yake hapa duniani. Kwa hiyo si suala la kuoa au kuolewa unavyotaka, bali ni kuoa au kuolewa kwa mapenzi yake.
  • Mapenzi ya Mungu si lazima yakubaliane/yaendane na ya kwako.
Ni muhimu ujue kwamba mapenzi ya Mungu si lazima yaendane na ya kwako. Na hii ni kwa sababu mawazo yako si mawazo yake na njia zake si njia zako (Isaya 55:8). Jua kabisa mapenzi ya Mungu si lazima yakupendeze, yakufurahishe au yalinde heshima yako.
  • Kuna nyakati ambazo mapenzi ya Mungu kuyapokea ni machungu, yanaliza, yanafadhaisha, yanaogopesha.
Katika kuyakubali au kuruhusu mapenzi ya Mungu yatimie wakati mwingine     yanaweza kuwa machungu, kukufadhaisha, kukuliza, kukuumiza, kukuogopesha au hata kukuabisha kwa jinsi ya kibinadamu.
  • Mapenzi ya Mungu yanalenga kuleta heshima na utukufu kwake.
Ingawaje yanaumiza, kufadhaisha au hata kuaibisha kwa jinsi ya kibidamu /kiheshima/kimahusiano/kijamii /kiuchumi nk. Na hata kama  kwako yana athari kiasi gani uwe na uhakika mapenzi ya Mungu yanalenga kuleta heshima na utukufu kwake, hii ina maana HAYO NDIYO MAPENZI YAKE na si ya KWAKO. Tunapoomba kusema mapenzi yako (Mungu) yatimizwe ina maana mapenzi/matakwa ya kwetu (wanadamu) yasitimie.
Hebu tuangalie mifano kadhaa ndani ya Biblia;
Mfano wa Yakobo - Mwanzo 29:15-31.
Hii ni habari ya Yakobo alipokwenda Harani kwa Labani nduguye. Labani alikuwa na binti wawili, mkubwa aliitwa Lea na mdogo aliitwa Raheli amabye alikuwa na uso na umbilie zuri. Raheli ndiye ambaye Yakobo alimpenda na alikubali kutumika kwa miaka saba ili apate kumuoa. Baada ya miaka saba, Yakobo alipewa Lea ambaye hakumpenda kama mke bali alimpenda Raheli. Ingawa zilipopita siku saba ndipo alipopewa na Raheli kama mke wa pili.
Nikuulize swali, je Yakobo angeambiwa atumike miaka saba kwa ajili ya kumpata Lea, angekubali? Je unafikiri ni kwa nini Mungu aliruhusu Yakobo  mtumishi wake kufanyiwa hili? Sababu kubwa ni hii, ilikuwa ni mpango/mapenzi ya Mungu Yakobo amuoe na Lea pia. Hii ni kwa sababu ya umuhimu wa watoto aliowazaa ukihusianisha na uzao/ukoo wa Bwana wetu Yesu Kristo. Namaanisha kupitia Lea, Yakobo alizaa naye watoto wane, mmoja wao aliitwa  Yuda. Ukifuatilia ukoo wa Yesu Kristo utalikuta jina la Yuda linajitokeza (Mathayo 1:2). Kwa hiyo japo Yakobo hakumpenda Lea kabisa lakini Mungu alitaka na akajua kupitia wao atazaliwa Yuda ambaye ni kiungo muhimu katika uzao wa Yesu Kristo.
Mfano wa nabii Hosea – Hosea 1:1-4
Mstari wa pili unasema ‘… Bwana alimwambia Hosea enenda ukatwae mke wa uzinzi…’ Ukisoma hii habari yote utaona jinsi Mungu alivyomwagiza Hosea kwenda kuoa mawanamke mzinzi na aliyekubuhu kwenye dhambi hii. Sasa kwa jinsi ya kibinadamu haikuwa rahisi kulikubali. Lakini kwa sababu ilikuwa ni jambo la MAPENZI YA MUNGU ili mlazimu akubaliane nalo hata kama yeye hakutaka. Na ukiendelea kusoma sura za mbele utaona fundisho na uponyaji ambao ulitokea kwa watu wa taifa la nabii Hosea kutokana na utiifu wake katika mapenzi ya Mungu.
 Mfano wa nabii Samweli – 1Samwel 16:1-13.
Hii ni habari inayoelezea agizo la Mungu kwa Samweli kwenda kwenye nyumba ya Yese kumtia mmoja wa watoto wake mafuta kuwa mfalme wa Israel baada ya Mfalme Sauli kuasi. Yese alikuwa na jumla ya wana nane wa kiume, Mkubwa  wao aliitwa Eliabu na mdogo aliitwa Daudi. Sasa Samweli alipofika kwa Yese, Yese aliwaita watoto wake wote isipokuwa Daudi aliyekuwa anachunga kondoo wa babaye, akaanza kuwapitisha kwa Samweli ili amtie mafuta yule ambaye ndio mfalme.
Alipopita mtoto wa kwanza, nabii Samweli akasema moyoni mwake Yakini masihi wa Bwana yupo hapa mbele yake, kwa lugha nyepesi alisema yamkini huyu ndiye Mfalme ninayepaswa kumtia mafuta. Je Mungu alimjibu nini alipowaza hivyo moyoni mwake. Mungu alimwambia ‘usimtazame uso wake, wala urefu wa kimo chake; kwa maana mimi nimemkataa. Bwana haangalii kama mwanadamu aangaliavyo; maana wanadamu huitazama sura ya nje, bali Bwana huutazama moyo’. Mwishowe walipita watoto wote saba na Bwana akawakataa, hadi alipofika Daudi aliyetiwa mafuta.
Jifunze yafuatayo kutoka kwenye mifano hii mitatu;
  • Upo duniani sasa kwa ridhaa/ruhusa/mapenzi ya Mungu.
  • Na kama upo kwa ridhaa yake, ni lazima uishi kwa uongozi wake (Zab 32:8).
  • Thamani ya maisha yako ipo katika kuyatenda mapenzi ya Mungu.
  • Ni kipaumbele (priority) cha Mungu kujua nani atakuwa ni mkeo au mumeo. Sio suala la kuoa au kuolewa unayotaka wewe.
  • Mtazamo wako kuhusu mkeo au mumeo sio mtazamo wa Mungu. Ndoa yoyote anayo iunganisha Mungu ameshaiangalia mpaka mwisho wake.
  • Hivyo anapokupa mtu wa aina fulani, hata kama haendani na vigezo vyako, kumbuka lengo lake sio kukukomoa au kukuhuzunisha bali ni kuhakikisha anachotaka/mapenzi yake na si ya kwako yanatimia.
  • Smweli na Yakobo walitaka kukosea kwa sababu ya maumbile na mvuto wa sura kwa nje. Angalia sababu kama hizi zisikufanye ukaharibu mahusiano yako na Mungu na hivyo kukwamisha makusudi yake duniani.
  • Japo lilikuwa ni jambo gumu kwa Hosea kulikubali kibinadamu, yeye alitii na akabarikiwa kwa kulitumikia shauri la Bwana katika kizazi chake.
  • Ni mfano wa mfinyanzi na vyombo alivyovifanya. Mfinyazi ndiye anayejua sababu na matumizi ya chombo alichokifanya. Kazi yake huyu mfinyazi ni kuhakikisha lengo la ubunifu/uumbaji wake linafikiwa.
  • Na Mungu ndivyo alivyo, yeye ndiye aliyekufanya na anajua unachotakiwa kufanya hapa dunani, kazi yake ni kuhakikisha anakuongoza na kukuweka kwenye mazingira ya kusudi lake kupitia wewe kufanikiwa. Sasa mazingira au uongozi huo ni pamoja na kuhakikisha unaoa au kuolewa na mtu wa mapenzi yake.
  • Mtu wa mapenzi yake anaweza akawa tofauti na ulivyokuwa unataka. Ndugu yangu inapofika uko mahali kama hapa “the only option/alternative ni kuruhusu mapenzi yake yatimie na si kulazimisha yako kutimia”. This means there is no an option or alternative, you cannot escape it (Je unakumbuka habari za Yona, au Yesu pale Gethesemane?). Let his will be made in your life i.e.   Totally submit yourself to his will.
  • Usipokubali wakati una hakika hayo ni mapenzi ya Mungu kwako maana yake umeasi, ukiasi unatafuta matakwa yako na si yake. Mungu hata kulazimisha kuyatii mapenzi yake ila atakushauri kwa njia mbalimbali na mojawapo na mafundisho kama haya. Ukikataa ushauri wake ujue huko unakoenda yeye/uwepo wake hauko pamoja na wewe. Je unajua gharama ya kukosea au kutokutii mapenzi ya Mungu katika hili? Waulize wanandoa waliokosea ndio utajua madhara yake.
  • Naamini ujumbe huu umekuongezea maarifa na ufahamu wa kukusaidia katika kufanya maamuzi. Zaidi ni imani yangu kwamba kama ukijua hakika haya ni mapenzi ya Mungu kuhusu mwenzi wako basi utahakikisha yanatimia. Haijalishi hayuko unavyotaka, ndugu zako, ukoo wako, kanisa au hata Mchungaji wako hawamtaki, kama unahakika ni mtu wa mapenzi ya Mungu mpendwa nakushauri RUHUSU MAPENZI YA MUNGU YATIMIE, KINYUME CHA HAPO NI MAJUTO.
  • “Asomaye na afahamu, msukumo ambao nimeupata kuhusu kuandika ujumbe huu haukuwa mdogo, ni kama nilikuwa naambiwa hakikisha ujumbe huu unakamilika haraka iwezekanavyo ili kuwapa maarifa haya watu wangu”.
 Mwenye sikio na asikie lile ambalo Roho wa Yesu anasema na kanisa. Amen.

E, WEWE NI MTUMWA WA MAPENZI?



Kuishi kama mtumwa wa ni hatari na huweza kupunguza hata ufanisi wako wa kazi. Kwanza kabla hatujafika mbali, hebu tuangalie maana ya utumwa wa mapenzi.
MAANA YA UTUMWA WA MAPENZI!
Hii ina maana pana sana, lakini naweza kutoa moja kama mjumuisho wa yote! Utumwa wa mapenzi unaweza kutokea pale, utakapompenda mtu ambaye hana habari na wewe kabisa, yaani unajikuta ukioza juu yake, lakini anakuwa hana mapenzi na wewe kabisa.
Wakati mwingine unaweza ukamshawishi mtu huyo kwa vitu fulani, akakubali kuwa na wewe lakini sio kwa mapenzi ila kwa kuwa kuna kitu fulani atapata kutoka kwako.
Kama ukiruhusu utumwa wa mapenzi, maisha yako ya kawaida, yanaweza kuharibika na kukosa muelekeo! Uwezo wako wa kufikiria utakuwa mdogo ma hata wakati mwingine kupunguza ufanisi wako wa kazi.
Muda mwingi utautumia kufikiri kwanini fulani hakuipendi? Una kasoro gani n.k, kimsingi kama ukiruhusu utumwa wa mapenzi, mpangilio wa maisha yako unaweza kuharika na kukosa muelekeo kabisa.
UTAJUAJE KAMA WEWE NI MTUMWA?
Hili ni rahisi kutambua ingawa ni hatua mbaya sana katika maisha yako. Jambo la kwanza ni mabadiliko ya hisia za moyo wako, utajikuta ukimpenda mtu sana, ambaye hata time kabisa na wewe! Pamoja na kuwa anaonyesha kila dalili za kukuchukia lakini bado utahisi kumpenda na kumhitaji katika maisha yako.
Moyo wako huendele kuysisitiza kuwa huyo sio sahihi kwa maisha yako, lakini bado mtu huyo ataendelea kukuonyesha kila vibwanga vya kuchukiza. Sio jamboi la ajabu kuhiusi kufa kuliko kuendelea kuteseka kwa penzi la huyo ambaye haonyeshi kutambua thamani ya penzi lako.
UTUMWA WA MAPENZI
Kipengele hiki ni kama kiini cha mada hii, tunapozungumzia utumwa halisi wa mapenzi, ni pale ulipojitahidi kumshawishi mpenzi huyo, kwa kila njia ili nuweze kuwa naye! Inawezekana ulimshawishi kwa pesa na wakati mwingine, ndugu zake walimlazimisha kuishi na wewe, akaamua ingawa hakupenda.
Mnapokuwa mmeingia kwenye ndoa, hapo sasa ndipo utumwa hukamilika! Sio rahisi kutoka tena (hasa kwa Wakristo) lakini mume/mke huyo atakuonyesha kila aina ya vimbwanga kuthibitisha kuwa hana mapenzi na wewe.
Inawezekana ukahitaji haki yako ya ndoa lakini akawa mgumu kukupa, kwa sababu hakupendi! Alikuoa/olewa na wewe kwa sababu ya shinikizo na sio mapenzi, lakini kwa kuwa tayari unakuwa umeshazoeana naye inakuwa vigumu kumtoa moyoni mwako.
Wengi wao hufikikia hatua ya kuamua maamuzi ambayo sio sahihi, baadhi yao huchanganyikiwa na wengine huona bora kufa kuliko kufedheheka! Kimsingi utumwa wa mapenzi ni ugonjwa mbaya sana kisaikolojia.CHUNGUZA MOYO WAKE
Hakika utumwa wa mapenzi ni ugonjwa mbaya sana, kimsingi usiruhusu kabisa kuwa mtumwa wa mapenzi. Hilo linawezekana kwa kumchunguza moyo wa huyo umpendaye. Katika hali ya kawaida, ni jambo gumu kidogo lakini iunawezekana.Unaweza kuuchunguza moyo wake kwa kuangalia je, ni kweli naye anakupenda kama unavyompenda? Kuna wengine hushindwa kukuambia SIKUTAKI, lakini anaendelea kuwa na wewe, kukufanya chombo cha starehe na kukupotezea muda wako. Ni rahisi kumtambua.
Mwulize kwanini anakupenda? Akupe sababu hasa za mapenzi yake kwako, akikuambia anakupenda kwa sababu ya umbo au sura nzuri, tambua huyo sio mpenzi sahihi na huenda akakufikisha katika utumwa wa mapenzi. Anayekupenda, hukujibu kuwa, amekupenda kama ulivyo, anaamini wewe ni mhimnili wa maisha yake na maisha yake yatakuwa kamili akiwa wewe na sio kuzungumzia habari za ngono!Mara nyingi ukimpigia simu, huchelewa kupokea kwa kisingizio cha kazi nyingi, ukimwandikia sms ndio kabisa hajibu! Yote hiyo ni kwa sababu hakupendi! Hana msisimko wowote na wewe.
Kwanza kama anakupenda, hata kwenye simu yake atakuwa amekuwekea mlio (Ring tone) tofauti na wengine, hivyo ukipiga lazima ajue ni wewe na hata kama ana kazi nyingi kiasi gani anapaswa kupokea, kwa kuwa wewe ni muhimu kwake!KATAA KUWA MTUMWA
Ukiona niliyoanisha katika kipengele kilichopita, ujue kuwa hakupendi, sasa kama ndivyo, huna sababu ya kukubali kuwa mtumwa! Kataa kwa nguvu na ni bora ukajifunza jinsi ya kukabiliana na hali ya kuishi bila huyo uliyempenda, kuliko kuishi naye halafu akutese.
Vipo vitu vingi vitakavyokusaidia kuepukana na hali ya sononeko katika moyo wako na kuishi maisha yako peke, huku ukimsubiri aliye maalum kwa ajili yako! Kataa kabisa kuwa mtumwa maana maisha yako huweza kuharibika moja kwa moja.

Je tunajua nini kuhusu Freemasonry?



http://strictlygospel.files.wordpress.com/2010/01/freemasons.jpg?w=490
Kama wakristo tuliookoka, tunatakiwa kuchukua hatua gani?
Nanukuu ‘Freemasons wa Tanzania? Waliojitokeza waziwazi na kujitambulisha ni kina Chande “Andy Chande” ambao ni matajiri wafanyabiashara maarufu. Katika mahojiano aliyofanya na mwandishi Muhiddin Michuzi wa gazeti la Sunday News la tarehe 3 April 2005, Sir Andy Chande alikiri kuwa anao wanachama zaidi ya 3,000 (yeye mwenyewe ni District Grand Master), na kuwa wamekuwa wakishirikiana na Rais Yoweri Museveni, Makamu wa Rais wa Kenya Moody Awori, na Rais Mstaafu Ben Mkapa (hakutaka kutamka wazi kuwa ni wanachama, lakini wapo watu wengine wanaofahamu kuwa hao aliowataja ni wanachama wa hiyo kitu, pamoja na Mzee Mengi). Alitamka kuwa mtu yeyote akishajiunga na freemasonry hawezi kutoka tena, kwa maneno yake “Once a freemason, always a freemason”.
Tazama jibu la Sir Andy Chande alipoulizwa na Muhiddin Michuzi kuhusu yalipo makao makuu ya Freemasons nchini Tanzania: “It is located along Sokoine Drive, just behind the Kilimanjaro Hotel in Dar es Salaam. We have a licence to sell drinks to members; we have also been exempted by the government of Tanzania from registration We have the full blessings of the government. Once that building was about to be taken over for public purpose, but when I sent a memorandum to the State House, we got it back. You know, Mwalimu Julius Nyerere was not a Freemason, but he knew what Freemasonry is”.

HAWEZ KUNIOA SIYO TYPE YANGU



Nategemea barua hii itakukuta salama. Mimi ni msichana wa miaka 23. Nilifiwa na wazazi wangu wakati nikiwa na miaka minane. Bibi yangu alishindwa kunilipia shule hivyo nikawa nyumbani tu, bahati nzuri mvulana mmoja kijijini kwetu akanambia atanisaidia, wakati huo alikuwa anauza machungwa barabarani. Kweli alianza kunilipia shule, miaka yote, hatimae hata yeye akabadili kazi akaanza kuendesha daladala, na ameendelea kunilipia mpaka sasa niko chuo kikuu. Namshukuru Mungu kwa kunikutanisha na malaika kama huyu sijui siku hizi ningekuwa wapi
Tatizo langu ni kuwa anataka kunioa nikimaliza chuo, na mimi kwa kweli nashindwa kumwambia kuwa itakuwa vigumu kwa kuwa yeye siyo 'type' yangu. Hebu fikiria mimi ni graduate halafu naolewa na dreva wa daladala, ni wazi kuwa si type yangu. Ninachoomba ni busara zako ntamwambiaje bila kumuumiza, kuwa haiwezekanai mimi nikaolewa na yeye?